June 21, 2018 Mbunge wa Temeke Abdallah Mtolea alisimama Bungeni ili kuchangia mapendekezo ya bajeti kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2018/19 ambapo amelieleza Bunge kuwa awamu ya tano ya uongozi imeongeza mfumuko wa bei wa bidhaa ikiwemo sukari na kuwasababishia wananchi hali ngumu ya kimaisha.