JAMBAZI SUGU WALIOMJERUHI MEJA JENERALI WAUWA

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dsm mnamo tarehe 11.10.2017 majira ya saa nne kamili usiku huko maeneo ya Mbezi Mshikamano kwa Mgalula, askari walipata taarifa kutoka kwa FRANCIS MINDE miaka 30, mfanyabiashara ambaye anamiliki duka la vitu mchanganyiko kwamba walifika watu wawili katika duka lake wakitumia pikipiki aina ya Boxer nyeusi ambayo haikusomeka namba na kumuuliza kama kuna huduma ya M-PESA na TIGO-PESA na kuwajibu kuwa hakuna huduma hiyo, aliwatilia mashaka huenda sio watu wazuri hatimaye alitoa taarifa Polisi.